Siku ya Sita

*Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.*

Nafahamu kuwa sababu ya dhambi zangu sala zangu zimefunikwa na wingu zisiweze kufika katika kiti chako cha enzi. Dhambi zangu ni sababu ya adhabu zangu kubwa. Sina ujasiri wa kuelekeza sauti yangu kwa Yesu. Kwa kuwa mara nyingi sikuthamini huruma yake. Na sasa naiona nguvu yake kuu na ya haki. Mkono wake wa haki umenielekea. Natambua kwamba sistahili baraka za msamaha wake kwani nimegubikwa na huzuni kubwa. Pasipo matumaini ninayalilia madhambi yangu. Niambie Mtakatifu Rita; Je, niendelee kukata tamaa? Hapana. Bwana wetu Yesu Kristo amekuteua kuwa mtetezi wake mwenye nguvu, ili uniombee kwa Yesu wangu aliye juu, msamaha kwa makosa yangu makubwa na nia safi ya kutomtendea dhambi tena. Kwa uamuzi huu thabiti, wa midomo yangu na moyo wangu, nakuelekea wewe. Ee Mtakatifu mtenda miujiza, uniombee kwa Bwana Yesu, fadhila ambazo nazihitaji sana **(hapa omba hitaji lako unalotaka kumwomba Mungu kupitia Mtakatifu Rita).**
Katika muda huu wa uchovu mkubwa, huzuni na kuachwa pweke; Ee Rita, neno lako kwa Yesu litafungua huruma na msamaha wake. Sema neno na Yesu atakusikia.

*Baba Yetu (3), Salamu Maria (3), Atukuzwe Baba (3)*

Kwa njia ya Mtakatifu Rita:- homa, madonda na tauni, viini vya maradhi mbalimbali, mapepo na ghadhabu vitoweke. *Unawasaidia vipofu, viziwi, bubu na viwete: watoto wanaomba sana na wafu wanarudishiwa uhai.*

Kwa maombezi yako:- radi, tetemeko la ardhi na moto havina nguvu. Kwa utakatifu wako mitego yote, hatari kubwa na vitisho vyote hutoweka. *Unawasaidia vipofu, viziwi, bubu na viwete: watoto wanaomba sana na wafu wanarudishiwa uhai.*

Hispania wanakutangaza kuwa Mtakatifu wa mambo yaliyoshindikana. Watu wengi wanaimba sifa zako. Kashia hutukuza jina lako. *Unawasaidia vipofu, viziwi, bubu na viwete: watoto wanaomba sana na wafu wanarudishiwa uhai.*

Kwa Mungu Mtakatifu, na kwa Mwanae ziwe sifa, utukufu na heshima, sifa kwa karne zote za pendo la milele. *Unawasaidia vipofu, viziwi, bubu na viwete: watoto wanaomba sana na wafu wanarudishiwa uhai.*

*K: Umemtia alama, Ee Bwana, mtumishi wako Rita.*
*W: Kwa mhuri wa upendo na mateso.*

*TUOMBE:* Ee Mungu, uliyekubali kumtawadha Mtakatifu Rita kwa neema, hata akakubali kuwapenda adui zake hadi akapata rohoni mwake na katika paji la uso alama za upendo na mateso. Tunakuomba kupitia maombezi yake, neema za kusamehe adui zetu na kutafakari maumivu ya mateso yako, ili tupate tuzo ulilotuahidia kwa wapole na wanaoteseka. Unayeishi na kutawala, daima na milele. Amina.

Baada ya kumaliza sehemu hii, sali Litania ya Mt. Rita, Litania ya Mwiba wa Mt. Rita, Zaburi ya 51 au Zaburi 130