Siku ya 5

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.

"Leo uniletee ROHO ZA WALE WALIOJITENGA NA KANISA LANGU, na uwazamishie katika bahari ya huruma yangu. Wakati wa Mateso yangu makali waliurarua Mwili na Moyo wangu, yaani Kanisa langu. Wanaporudi katika umoja na Kanisa, majeraha yangu hupona na kwa njia hii wanapunguza Mateso yangu."

Yesu Mwenye Huruma Sana, Wema wenyewe, huwanyimi mwanga wale wanaoutafuta kwako. Zipokee katika makao ya Moyo wako wenye Huruma Sana roho za wale waliojitenga na Kanisa lako. Wavute kwa mwanga wako katika umoja wa Kanisa, wala usiwaache watoke katika makao ya Moyo wako wenye Huruma Sana; bali ufanye kwamba wao pia waje kuitukuza ukarimu wa huruma yako.

Baba wa Milele, elekeza macho yako ya huruma juu ya roho za wale waliojitenga na Kanisa la Mwanao, ambao wamepoteza baraka zako na kutumia vibaya neema zako kwa kung'ang'ania kwa ukaidi makosa yao. Usitazame makosa yao, bali tazama upendo wa Mwanao mwenyewe na Mateso yake makali aliyoyavumilia kwa ajili yao, kwa kuwa wao pia wamefungiwa ndani ya Moyo wake wenye Huruma Sana. Fanya kwamba wao pia waweze kuitukuza huruma yako kuu kwa nyakati zisizo na mwisho.

Amina.

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.