Siku ya 3

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.

"Leo uniletee ROHO ZOTE ZA WAUMINI WACHAMUNGU NA WAAMINIFU, na uwazamishie katika bahari ya huruma yangu. Roho hizi ziliniletea faraja katika Njia ya Msalaba. Zilikuwa tone la faraja katikati ya bahari ya uchungu."

Yesu Mwenye Huruma Sana, kutoka hazina ya huruma yako, unatoa neema zako kwa wingi mkubwa kwa kila mmoja na kwa wote. Utupokee katika makao ya Moyo wako wenye Huruma Sana wala usituache kamwe tutoke humo. Tunakuomba neema hii kwa ule upendo wa ajabu kabisa kwa Baba wa mbinguni ambao Moyo wako huwaka nao kwa nguvu sana.

Baba wa Milele, elekeza macho yako ya huruma juu ya roho za waaminifu, kama juu ya urithi wa Mwanao. Kwa ajili ya Mateso yake yenye uchungu, uwajalie baraka yako na uwazungushie ulinzi wako wa daima. Hivyo wasianguke kamwe katika upendo wala kupoteza hazina ya imani takatifu; bali, pamoja na majeshi yote ya Malaika na Watakatifu, waitukuze huruma yako isiyo na mipaka kwa nyakati zisizo na mwisho.

Amina.

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.