Siku ya 2

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.

"Leo uniletee ROHO ZA MAPADRE NA WATAWA, na uwazamishie katika huruma yangu isiyopimika. Hao ndio walionipa nguvu ya kuvumilia Mateso yangu makali. Kupitia kwao, kama kupitia mifereji, huruma yangu hutiririka juu ya wanadamu."

Yesu Mwenye Huruma Sana, ambaye kutoka kwako hutoka mema yote, ongeza neema yako kwa wanaume na wanawake waliowekwa wakfu kwa huduma yako, ili watende matendo ya huruma yanayostahili; na ili wote wanaowaona wamtukuze Baba wa Huruma aliye mbinguni.

Baba wa Milele, elekeza macho yako ya huruma juu ya kundi la wateule katika shamba lako la mizabibu, yaani juu ya roho za mapadre na watawa; na uwajalie nguvu ya baraka yako. Kwa upendo wa Moyo wa Mwanao ambamo wamefunikwa, uwape uwezo wako na mwanga wako, ili waweze kuwaongoza wengine katika njia ya wokovu na kwa sauti moja waimbe sifa za huruma yako isiyo na mipaka milele na milele.

Amina.

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.