Siku ya 8

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.

"Leo uniletee ROHO ZINAZOZUILIWA TOHARANI, na uwazamishie katika kina cha huruma yangu. Mifuriko ya Damu yangu ipoze miali yao inayowaka. Roho hizi zote zinapendwa sana nami. Zinalipa fidia kwa haki yangu. Iko katika uwezo wako kuziletea nafuu. Chota rehema zote kutoka hazina ya Kanisa langu na uzitoe kwa ajili yao. Laiti ungejua mateso wanayoyapata, ungeendelea kuwatoea sadaka za roho na kulipa deni lao kwa haki yangu."

Yesu Mwenye Huruma Sana, wewe mwenyewe umesema kwamba unatamani huruma; kwa hiyo ninazileta katika makao ya Moyo wako wenye Huruma Sana roho zilizo Toharani, roho zilizo karibu sana nawe, lakini ambazo bado zinapaswa kulipa fidia kwa haki yako. Mito ya Damu na Maji iliyobubujika kutoka Moyoni mwako izime miali ya Toharani, ili huko pia uwezo wa huruma yako uweze kusherehekewa.

Baba wa Milele, elekeza macho yako ya huruma juu ya roho zinazoteseka Toharani, ambazo zimefunikwa katika Moyo wa Yesu wenye Huruma Sana. Ninakuomba, kwa Mateso yenye uchungu ya Yesu Mwanao, na kwa uchungu wote ambao Nafsi yake takatifu kabisa ilifurika nao: Udhihirishe huruma yako kwa roho zilizo chini ya uchunguzi wako wa haki. Usiziangalie kwa njia nyingine yoyote ila tu kupitia Majeraha ya Yesu, Mwanao mpendwa sana; kwa maana tunaamini kwa uthabiti kwamba hakuna kikomo kwa wema na huruma yako.

Amina.

Sali Chapleti ya Huruma ya Mungu.

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.