Siku ya 9
Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
Amina.
Enyi watakatifu mliokuwa katika ndoa wakati wa maisha yenu duniani, ambao ndoa yenu duniani ilionyesha karamu ya arusi ya mbinguni, mlijua kukua katika utakatifu kupitia furaha na huzuni za maisha ya ndoa na familia. Niombeeni nitambue jambo la ajabu katika mwendo wa kawaida wa maisha ya familia. Ninaomba mziweke haja zangu mbele ya Mungu.
(Taja nia zako hapa)
Mtakatifu Maria na Mtakatifu Yosefu, wazazi wa Yesu, mtuombee.
Mtakatifu Ana na Mtakatifu Yoakimu, wazazi wa Bikira Maria, mtuombee.
Mtakatifu Elisabeti na Mtakatifu Zakaria, wazazi wa Mtakatifu Yohane Mbatizaji, mtuombee.
Mtakatifu Zelia Guerin Martin na Mtakatifu Louis Martin, wazazi wa Mtakatifu Teresia wa Lisieux, mtuombee.
Mtakatifu Nonna na Mtakatifu Gregori Mzee, wazazi wa Mtakatifu Gorgonia, Mtakatifu Caesarius, na Mtakatifu Gregori wa Nazianzus, mtuombee.
Amina.
Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
Amina.
Day 9
In the name of the Father, and of the Son, and of the Holy Spirit.
Amen.
O holy saints who were married during your earthly life, whose marriage on Earth prefigured the wedding feast in Heaven, you knew how to grow in holiness through the joys and sorrows of married and family life. Intercede on my behalf that I may recognize the extraordinary in the ordinary course of family life. I ask that you place before God my petitions.
(State your intentions here)
St. Mary and St. Joseph, parents of Jesus, pray for us.
St. Anne and St. Joachim, parents of the Blessed Virgin Mary, pray for us.
St. Elizabeth and St. Zechariah, parents of St. John the Baptist, pray for us.
St. Zelie Guerin Martin and St. Louis Martin, parents of St. Therese of Lisieux, pray for us.
St. Nonna and St. Gregory the Elder, parents of St. Gorgonia, St. Caesarius, and St. Gregory of Nazianzus, pray for us.
Amen.
In the name of the Father, and of the Son, and of the Holy Spirit.
Amen.