Siku ya 7

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.

Amina.

Enyi watumishi watakatifu na wanyenyekevu wa Mungu, mnaong’aa kwa utakatifu kupitia unyenyekevu wenu wa kweli, mlikubali utambulisho wenu kama vyombo vya Mungu. Niombeeni niondolewe ubinafsi na kutakaswa ili niwe chombo kilichowekwa wakfu kwa kazi ya Mungu. Ninaomba mziweke haja zangu mbele ya Mungu.

(Taja nia zako hapa)

Mtakatifu Bernadeta, utuombee.

Mtakatifu Teresia wa Lisieux, utuombee.

Mtakatifu Yosefu wa Cupertino, utuombee.

Mtakatifu Juan Diego, utuombee.

Watakatifu Fransisko na Jacinta de Jesus Marto, mtuombee.

Amina.

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.

Amina.