Siku ya 7
Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
Amina.
Bwana mpendwa, tunakushukuru kwa kutupatia Mtakatifu Aloysius Gonzaga kama mfano wa utakatifu. Utusaidie kuiga upendo aliokuonyesha kwa kujitoa kuwahudumia wagonjwa licha ya hatari kwa afya yake.
Mtakatifu Aloysius Gonzaga, ulikuwa na hamu ya kuwahudumia ndugu zako wanaoteseka katika Kristo, katikati ya janga baya. Ulidumu kuomba ruhusa ya kuwahudumia wagonjwa, ingawa ulijua jambo hilo lingeweza kuhatarisha afya yako.
Tafadhali dumu kuziwasilisha haja zangu mbele ya Mungu!
Kwa kawaida ulichukizwa na hali zisizopendeza za ugonjwa uliokuzunguka, lakini hata hivyo ulijitoa kwa moyo wote katika kazi ya kuwahudumia watu hawa wanaoteseka.
Uniombee, ili nisiruhusu hali zisizopendeza zinizuie kumtumikia Mungu. Omba daima nidumu kutafuta kumtumikia Mungu, licha ya vizuizi vyote.
Tafadhali ombea pia (taja nia zako hapa).
Mtakatifu Aloysius Gonzaga, utuombee!
Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
Amina.
Day 7
In the name of the Father, and of the Son, and of the Holy Spirit.
Amen.
Dear Lord, we thank You for giving us St. Aloysius Gonzaga as an example of holiness. Help us to imitate the love of You he showed in committing himself to care for the sick despite dangers to his own health.
St. Aloysius Gonzaga, you were eager to care for your suffering brothers and sisters in Christ, in the midst of a terrible epidemic. You persisted in seeking permission to care for the sick, even though you knew it might endanger your own health.
Please persist in bringing my petitions before God!
You felt natural revulsion toward the unpleasant realities of the sickness around you, but you wholeheartedly threw yourself into the task of caring for these suffering people anyway.
Pray for me, that I may never allow unpleasantness to deter me from serving God. Pray that I may always persevere in seeking to serve God, despite all obstacles.
Please also pray for (mention your intentions here).
St. Aloysius Gonzaga, pray for us!
In the name of the Father, and of the Son, and of the Holy Spirit.
Amen.