Siku ya 8

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.

Amina.

Litania ya Tumaini

Kutoka imani kwamba ni lazima niustahili upendo wako - Uniokoe, Yesu.

Kutoka hofu kwamba sistahili kupendwa - Uniokoe, Yesu.

Kutoka usalama wa uongo kwamba ninaweza yote kwa nguvu zangu - Uniokoe, Yesu.

Kutoka hofu kwamba kukutumainia kutaniacha maskini zaidi - Uniokoe, Yesu.

Kutoka mashaka yote juu ya maneno na ahadi zako - Uniokoe, Yesu.

Kutoka uasi dhidi ya kukutegemea kama mtoto - Uniokoe, Yesu.

Kutoka kukataa na kusita kuyakubali mapenzi yako - Uniokoe, Yesu.

Kutoka wasiwasi kuhusu siku zijazo - Uniokoe, Yesu.

Kutoka kinyongo au kushughulishwa kupita kiasi na yaliyopita - Uniokoe, Yesu.

Kutoka kujitafuta kusikotulia katika wakati huu wa sasa - Uniokoe, Yesu.

Kutoka kutokuamini upendo wako na uwepo wako - Uniokoe, Yesu.

Kutoka hofu ya kuombwa kutoa zaidi ya nilivyo navyo - Uniokoe, Yesu.

Kutoka imani kwamba maisha yangu hayana maana wala thamani - Uniokoe, Yesu.

Kutoka hofu ya madai ya upendo - Uniokoe, Yesu.

Kutoka kukata tamaa - Uniokoe, Yesu.

Kwamba daima unanishika, unanitegemeza, unanipenda - Yesu, nakutumainia.

Kwamba upendo wako huzama zaidi kuliko dhambi na mapungufu yangu na hunibadilisha - Yesu, nakutumainia.

Kwamba kutojua yatakayotokea kesho ni mwaliko wa kukuegemea - Yesu, nakutumainia.

Kwamba uko pamoja nami katika mateso yangu - Yesu, nakutumainia.

Kwamba mateso yangu, yakiunganishwa na mateso yako, yatazaa matunda katika maisha haya na yajayo - Yesu, nakutumainia.

Kwamba hutanilacha yatima, na kwamba upo katika Kanisa lako - Yesu, nakutumainia.

Kwamba mpango wako ni bora kuliko kitu kingine chochote - Yesu, nakutumainia.

Kwamba daima unanisikia na kwa wema wako daima unanijibu - Yesu, nakutumainia.

Kwamba unanipa neema ya kukubali msamaha na kuwasamehe wengine - Yesu, nakutumainia.

Kwamba unanipa nguvu zote ninazohitaji kwa yale ninayoombwa - Yesu, nakutumainia.

Kwamba maisha yangu ni zawadi - Yesu, nakutumainia.

Kwamba utanifundisha kukutumainia - Yesu, nakutumainia.

Kwamba wewe ni Bwana wangu na Mungu wangu - Yesu, nakutumainia.

Kwamba mimi ni mpendwa wako - Yesu, nakutumainia.

Kwamba utasikia sala zangu (taja nia zako hapa) - Yesu, nakutumainia.

Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.

Amina.