Litania ya Mama Yetu wa Mateso Saba

Litania ya kumheshimu Bikira Maria, Mama wa Mateso Saba, iliyoandikwa na Papa Pius VII.

Litania ya Mama Yetu wa Mateso Saba

Bwana, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Kristo, utuhurumie.
Kristo, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Kristo, utusikie.
Kristo, utusikilize.
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie.
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia, Utuhurumie.
Mungu Roho Mtakatifu, Utuhurumie.
Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja, Utuhurumie.

Kiitikio: Utuombee

Maria Mtakatifu Mama wa Mungu,
Bikira Mtakatifu wa Mabikira,
Mama wa Msulubiwa,
Mama mwenye uchungu mwingi,
Mama uliyejaa huzuni,
Mama mwenye majonzi,
Kioo cha uvumilivu,
Mwamba wa udumifu,
Dawa ya mfadhaiko,
Furaha ya wenye huzuni,
Safina ya waliotelekezwa,
Makimbilio ya wapweke,
Ngao ya wanaokandamizwa,
Mshindaji wa wasioamini,
Faraja ya wanyonge,
Dawa ya wagonjwa,
Mkingaji wa wapiganaji,
Bandari salama kwa meli iliyovunjika,
Mtuliza tufani,
Mwenzi wa wenye uchungu mwingi,
Kimbilio la walioelemewa,
Kitisho cha wasaliti,
Taji la Mashahidi,
Hazina bora ya waamini,
Mwanga wa Waungama,
Lulu bora ya Mabikira,
Mfariji wa Wajane,
Furaha ya Watakatifu wote,
Malkia wa Watumishi wako,
Maria Mtakatifu, ambaye ni pekee uliyefananishwa,
Utuombee.

K. Utuombee, Bikira mwenye Uchungu mwingi,
M. Ili tuweze kustahiki ahadi za Kristo.

TUOMBE:

Ee Mungu ambaye kwa mateso yake, kulingana na unabii wa Simeoni, upanga wa uchungu ulichoma moyo mtakatifu sana wa Bikira Maria, Mama yako mtukufu; utujalie sisi tunaokumbuka kwa heshima uchungu wake, tupate matunda yenye heri ya mateso yako. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.

litaniabikira mariamama yetumateso sabapapa pius vii

← Back to Litanies