Litania ya Malipizi

Litany ya kutoa malipizi kwa Mungu kwa niaba ya dhambi za ulimwengu, hasa dhambi dhidi ya Ekaristi Takatifu.

LITANIA YA MALIPIZI

Kwa ajili ya wagonjwa, wanaoteseka, na wote wanaofariki siku ya leo, hasa wale ambao hawakujiandaa kufa.

SALA KWA AJILI YA ROHO ZENYE SHIDA:

Baba wa milele, ninakutolea Damu Azizi ya Mwanao Yesu, kwa kuungana na Misa zote zinazosaliwa siku ya leo ulimwenguni kote, kwa ajili ya roho zote zilizoko Toharani, kwa ajili ya wakosefu mahali popote, kwa ajili ya wakosefu wa Kanisa Katoliki, na kwa ajili ya wale walio nyumbani kwangu na ndani ya familia yangu. Amina.

Bwana, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Kristo, utuhurumie.
Kristo, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Kristo, utusikie.
Kristo, utusikilize.
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie.
Mungu Mwana, Mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu, Utuhurumie.
Mungu Roho Mtakatifu, mwanga wa mioyo, Utuhurumie.
Utatu Mtakatifu na Usiogawanyika, Utuhurumie.

KAFARA YA MALIPIZI:

Hostia Takatifu, Kafara ya malipizi kwa ajili ya dhambi za ulimwengu, Utuhurumie.
Hostia Takatifu, inayotolewa Altareni na sisi kwa ajili yetu sisi, Utuhurumie.
Hostia Takatifu, inayodharauliwa na kutojaliwa, Utuhurumie.
Hostia Takatifu, inayofanyiwa jeuri na kufuru za watu, Utuhurumie.
Hostia Takatifu, inayotelekezwa na kuachwa katika Hekalu Zako, Utuhurumie.
Uturehemie, Utusamehe Bwana.
Uturehemie, Utusikilize Bwana.

MAOMBI YA MALIPIZI:

Katika makufuru ya makusudi kwa sakramenti hii ya ajabu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Katika komunyo zisizostahili, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa wakristo kukosea heshima, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya mazungumzo yanayofanyika katika mahekalu yako matakatifu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya dhambi za wakosefu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kufuru ya Sakramenti ya Mapendo, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya ubaridi wa watoto wako, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa kudharau mwaliko wako mpendevu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya ukosefu wa uaminifu wa wale wanaojiita rafiki zako, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kutotumia neema zako kwa ukamilifu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kutumia vibaya neema zako, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya ukosefu wa uaminifu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kuchelewa kwetu kukupenda, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya ulegevu katika utumishi wako Mtakatifu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kutokuwa mpendevu jinsi tunavyopaswa, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kukudharau, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kuwa na ufidhuli na kiburi, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kushindwa kutimiza wajibu wetu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kutotii Mapenzi yako Matakatifu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kutokutoa mfano mzuri, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kushindwa kujirekebisha makosa yetu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya uchungu unaopata kwa upotevu wa roho za watu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kusubiri kwa muda mrefu kwenye milango ya mioyo yetu, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya miguno yako ya upendo, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya machozi yako ya upendo, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kifungo chako cha upendo, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.
Kwa ajili ya kifo chako cha mapendo, Tunakutolea malipizi yetu, Ee Bwana.

MWISHO:

Utuokoe, utusikilize, Sisi wadhambi twakuomba utusikie.
Mapendo yako yajulikane kwa ajili yetu katika sakramenti takatifu, Sisi wadhambi twakuomba utusikie.
Ukubali kuyapokea malipizi yetu, tuliyofanya kwa roho za unyenyekevu, Sisi wadhambi twakuomba utusikie.
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za ulimwengu, Utusamehe Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za ulimwengu, Utusikilize Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za ulimwengu, Utuhurumie.

SALA YA MALIPIZI:

Utatu Mtakatifu sana, Baba, Mwana, Roho Mtakatifu, ninakuabudu kwa dhati na ninakutolea Mwili, Damu, Roho, na Umungu wa Yesu Kristo, vilivyo katika Tabernakulo zote za ulimwengu, kwa malipizi ya ujeuri, kufuru, na kutojali kwa hivyo anavyokosewa sana. Na kwa mastahili ya Moyo wake Mtakatifu sana, na kwa njia ya Moyo Safi wa Maria, ninakuomba uongofu wa wakosefu maskini. Amina.

litaniamalipiziekaristisakramentitoba

← Back to Litanies