Litania ya Malaika Watakatifu
Litania ya kuomba maombezi na ulinzi wa Malaika watakatifu.
Litania ya Malaika Watakatifu
Bwana, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Kristu, utuhurumie.
Kristu, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Kristu, utusikie.
Kristu, utusikilize.
Kiitikio: Utuhurumie
Mwana, Mkombozi wa dunia, Mungu,
Roho Mtakatifu, Mungu,
Utatu Mtakatifu, Mungu mmoja,
Kiitikio: Utuombee
Maria Mtakatifu, Malkia wa Malaika,
Mzazi Mtakatifu wa Mungu,
Bikira Mtakatifu wa mabikira,
Mtakatifu Mikaeli, ambaye daima ulikuwa mtetezi wa watu wa Mungu,
Mtakatifu Mikaeli, uliyemfukuza kutoka mbinguni Lusifa na kundi lake la waasi,
Mtakatifu Mikaeli, uliyemtupa kuzimu mshitaki wa ndugu zetu,
Mtakatifu Gabrieli, uliyemfafanulia Danieli maono ya mbinguni,
Mtakatifu Gabrieli, uliyemtangazia Zakaria kuzaliwa na huduma ya Yohane Mbatizaji,
Mtakatifu Gabrieli, uliyemtangazia Maria Mtukufu Umwilisho wa Neno wa Mungu,
Mtakatifu Rafaeli, uliyemwongoza Tobia salama katika safari yake kurudi nyumbani,
Mtakatifu Rafaeli, uliyemwokoa Sara kutoka kwa shetani,
Mtakatifu Rafaeli, uliyemrudishia Tobia mzee kuona,
Enyi Malaika watakatifu wote, msimamao kuzunguka kiti cha enzi cha juu na kitukufu cha Mungu,
Mnaomlilia daima: Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu,
Mnaoondoa giza la akili zetu na kutupa nuru,
Mlio wajumbe wa mambo ya mbinguni kwa wanadamu,
Mliowekwa na Mungu kuwa Walinzi wetu,
Mnaouona daima Uso wa Baba yetu aliye mbinguni,
Mnaofurahi juu ya mkosefu mmoja anayetubu,
Mliowapiga Wasodoma kwa upofu,
Mliomtoa Lutu kati ya wasiomcha Mungu,
Mliopanda na kushuka katika ngazi ya Yakobo,
Mliomletea Musa Sheria ya Mungu juu ya Mlima Sinai,
Mlioleta habari njema Kristu alipozaliwa,
Mliomhudumia jangwani,
Mliomfariji katika uchungu wake,
Mlioketi katika mavazi meupe kwenye kaburi lake,
Mliowatokea wanafunzi alipokuwa akipaa mbinguni,
Mtakaomtangulia mkibeba bendera ya Msalaba atakapokuja kuhukumu,
Mtakaowakusanya wateule mwisho wa dunia,
Mtakaowatenga waovu kutoka kati ya wenye haki,
Mnaomtolea Mungu sala za wanaosali,
Mnaotusaidia saa ya kufa,
Mliomchukua Lazaro katika kifua cha Abrahamu,
Mnaoongoza roho za wenye haki kwenda mbinguni,
Mnaotenda ishara na maajabu kwa nguvu ya Mungu,
Mnaotumwa kuhudumia wale watakaopokea urithi wa wokovu,
Mliowekwa juu ya falme na majimbo,
Mliovikimbiza mara nyingi vikosi vya maadui,
Mliowaokoa mara nyingi watumishi wa Mungu kutoka gerezani na hatari nyingine za maisha haya,
Mliowafariji mara nyingi mashahidi watakatifu katika mateso yao,
Mnaowatunza kwa uangalifu wa pekee Maaskofu wa Kanisa,
Enyi makundi yote matakatifu ya roho wabarikiwa,
Kiitikio: Utuokoe, ee Bwana
Kutoka hatari zote,
Kutoka mitego ya shetani,
Kutoka uzushi wote na mafarakano,
Kutoka tauni, njaa na vita,
Kutoka kifo cha ghafla na kisichotarajiwa,
Kutoka kifo cha milele,
Kiitikio: Tunakuomba utusikilize
Sisi wakosefu,
Kwa njia ya Malaika watakatifu,
Ili upende kutusamehe,
Ili upende kutuachilia,
Ili upende kuliongoza na kulihifadhi Kanisa lako Takatifu,
Ili upende kumlinda askofu wetu na wahudumu wote wa Kanisa,
Ili upende kuwajalia watawala wote wa nchi amani na usalama,
Ili upende kutoa na kuhifadhi matunda ya nchi,
Ili upende kuwajalia mapumziko ya milele marehemu wote waamini,
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia,
Utusamehe, ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia,
Utusikilize kwa huruma, ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia,
Utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Kristu, utuhurumie.
Bwana, utuhurumie.
Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe; Ufalme wako ufike, Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni. Utupe leo riziki yetu, utusamehe makosa yetu kama tunavyowasamehe waliotukosea; wala usitutie majaribuni, lakini utuopoe maovuni. Amina.
Mhimidini Bwana, enyi Malaika wake wote: Ninyi mlio hodari kwa nguvu, mnaotimiza amri zake, mkisikiliza sauti ya maneno yake.
Amewaamuru Malaika wake wakulinde,
Wakulinde katika njia zako zote.
Tuombe.
Ee Mungu, upangaye huduma za Malaika na wanadamu kwa utaratibu wa ajabu, utujalie kwa huruma kwamba maisha yetu duniani yalindwe na wale wanaokutumikia daima mbinguni, kwa njia ya Yesu Kristu Mwanao, ambaye pamoja nawe na Roho Mtakatifu ni Mungu mmoja, sasa na milele. Amina.
Ee Mungu, ambaye kwa maongozi yako yasiyosemeka huwatuma Malaika wako watulinde, utujalie tutetewe daima na ulinzi wao na kufurahi milele katika ushirika wao, kwa njia ya Yesu Kristu Bwana wetu, aishiye na kutawala nawe katika umoja wa Roho Mtakatifu, milele na milele. Amina.
Litany of the Holy Angels
A litany invoking the intercession and protection of the holy angels.
Litany of the Holy Angels
Lord have mercy.
Lord have mercy.
Christ have mercy.
Christ have mercy.
Lord have mercy.
Lord have mercy.
Christ hear us.
Christ graciously hear us.
Response: Have mercy on us
God the Son, Redeemer of the world,
God the Holy Spirit,
Holy Trinity, One God,
Response: Pray for us
Holy Mary, Queen of Angels,
Holy Mother of God,
Holy Virgins of virgins,
Saint Michael, who was ever the defender of the people of God,
St. Michael, who did drive from Heaven Lucifer and his rebel crew,
St. Michael, who did cast down to Hell the accuser of our brethren,
Saint Gabriel, who did expound to Daniel the Heavenly vision,
St. Gabriel, who did foretell to Zachary the birth and ministry of John the Baptist,
St. Gabriel, who did announce to the Blessed Mary the Incarnation of the Divine Word,
Saint Raphael, who did lead Tobias safely through his journey to his home again,
St. Raphael, who did deliver Sara from the devil,
St. Raphael, who did restore sight to Tobias the elder,
All ye holy Angels, who stand around the high and lofty throne of God,
Who cry to Him continually: Holy, Holy, Holy,
Who dispel the darkness of our minds and give us light,
Who are the messengers of Heavenly things to men,
Who have been appointed by God to be our Guardians,
Who always behold the Face of our Father Who Is in Heaven,
Who rejoice over one sinner doing penance,
Who struck the Sodomites with blindness,
Who led Lot out of the midst of the ungodly,
Who ascended and descended on the ladder of Jacob,
Who delivered the Divine Law to Moses on Mount Sinai,
Who brought good tidings when Christ was born,
Who ministered to Him in the desert,
Who comforted Him in His agony,
Who sat in white garments at His sepulcher,
Who appeared to the disciples as He went up into Heaven,
Who shall go before Him bearing the standard of the Cross when He comes to judge,
Who shall gather together the elect at the End of the World,
Who shall separate the wicked from among the just,
Who offer to God the prayers of those who pray,
Who assist us at the hour of death,
Who carried Lazarus into Abraham's bosom,
Who conduct to Heaven the Souls of the just,
Who perform signs and wonders by the power of God,
Who are sent to minister for those who shall receive the inheritance of salvation,
Who are set over kingdoms and provinces,
Who have often put to flight armies of enemies,
Who have often delivered God's servants from prison and other perils of this life,
Who have often consoled the holy Martyrs in their torments,
Who cherish with particular care the Bishops of the Church,
All ye holy orders of blessed spirits,
Response: Deliver us, O Lord
From all dangers,
From the snares of the devil,
From all heresy and schism,
From plague, famine and war,
From sudden and unexpected death,
From everlasting death,
Response: We beseech Thee to hear us
We sinners,
Through the holy Angels,
That Thou wouldst spare us,
That Thou wouldst pardon us,
That Thou wouldst govern and preserve Thine Holy Church,
That Thou wouldst protect our bishop and all ministers of the Church,
That Thou wouldst grant peace and security to all country rulers,
That Thou wouldst give and preserve the fruits of the earth,
That Thou wouldst grant eternal rest to all the Faithful departed,
Lamb of God, Who takes away the sins of the world,
Spare us, O Lord.
Lamb of God, Who takes away the sins of the world,
Graciously hear us, O Lord.
Lamb of God, Who takes away the sins of the world,
Have mercy on us.
Lord have mercy.
Christ have mercy.
Lord have mercy.
Our Father Who Art in Heaven, hallowed be Thy Name; Thy Kingdom come, Thy Will be done, on earth as it is in Heaven. Give us this day our daily bread and forgive us our trespasses as we forgive those who trespass against us; and lead us not into temptation, but deliver us from evil, Amen.
Bless the Lord, all ye Angels: Thou who art mighty in strength, who fulfill His commandments, listening to the voice of His words.
He has given His Angels charge over you,
To keep you in all His ways.
Let Us Pray.
O God, Who doth arrange the services of Angels and men in a wonderful order, mercifully grant that our life may be protected on earth by those who always do Thy service in Heaven, through Jesus Christ Thy Son, Who with Thee and the Holy Spirit are one God, now and forever. Amen.
O God, Who in Thine unspeakable Providence sends Thy Angels to keep guard over us, grant us that we may be continually defended by their protection and may rejoice eternally in their company, through Jesus Christ Our Lord, Who livest and reignest with Thee, in the unity of the Holy Spirit, forever and ever. Amen.