Sala ya Jioni
Mpangilio wa sala za jioni pamoja na shukrani, ungamo la dhambi, toba, Angelus, na sala kwa Malaika Mlinzi.
SALA YA JIONI.
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina.
Tunakushukuru ee Mungu kwa mema yote uliyotujalia sikuu hii ya leo.
BABA YETU.
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku. Utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina.
SALAMU MARIA.
Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
SALA YA IMANI.
Mungu wangu, nasadiki maneno yote. Linayosadiki na linayofundisha Kanisa Katoliki la Roma. Kwani ndiwe uliyetufumbulia hayo. Wala hudanganyiki, wala hudanganyi. Amina.
SALA YA MATUMAINI.
Mungu wangu, natumaini kwako, nitapewa kwa njia ya Yesu Kristo. Neema zako hapa duniani, na utukufu mbinguni. Kwani ndiwe uliye agana hayo nasi, nawe mwamini. Amina.
SALA YA MAPENDO.
Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote. Kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu, kama nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina.
UNGAMO LA DHAMBI.
Na tuwaze katika moyo makoda yote ya leo tuliyomkosea Mungu, kwa mawazo, kwa maneno na kwa matendo(………………………)
Namuungamia Mungu Mwenyezi, nanyi ndugu zangu, kwani nimekosa mno, kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo na kwa kutokutimiza wajibu, nimekosa mimi, nimekosa mimi, nimekosa sana. Ndio maana nakuomba Maria mwenyeheri, Bikira daima, malaika na watakatifu wote, nanyi ndugu zangu, niombeeni kwa Bwana Mungu wetu.
+Mungu Mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi zetu na atufukishe kwenye uzima wa milele, Amina.
SALA YA KUTUBU.
Mungu wangu, nimetubu sana niliyokosa kwako. Kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Wachukizwa na dhambi, basi sitaki kukosa tena. Nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi. Amina.
Ee Mungu mwenye huruma, uwashushie baraka zako, Baba Mtakatifu wetu Francis na maaskofu, na mapadre, na mashemasi, wakulima, wafanyakazi wote, wanafunzi na jamii yote unaowafanya kuwa watu wako . Uwaokoe washenzi, uwafariji wagonjwa, waelekee wanaozimia waweze kuona mwanga wa milel, Amina.
ANGELUS.
Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria,naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Ndimi mtumishi wa Bwana,nitendewe ulivyosema.
~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Neno wa Mungu akatwaa mwili,akakaa kwetu.
~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Utuombee mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe:
Tunakuomba ee Bwana utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya malaika, kwamba Kristo mwanao amejifanya mtu; kwa mateso na msalaba wake, tufikishwe kwenye utukufu na ufufuko.
Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
Bikira Maria Malkia wa amani~Utuombee!
SALA KWA MALAIKA MLINZI.
Malaika mlinzi wangu, unilinde katika hatari zote, za roho na za mwili. Amina.
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina
Evening Prayer
An evening prayer order with thanksgiving, confession, contrition, Angelus, and guardian angel prayer.
EVENING PRAYER.
In the name of the Father, and of the Son, and of the Holy Spirit. Amen.
We thank you, O God, for all the good things you have given us this day.
OUR FATHER.
Our Father, who art in heaven, hallowed be thy name. Thy kingdom come. Thy will be done on earth as it is in Heaven.
Give us this day our daily bread. Forgive us our trespasses, as we forgive those who trespass against us. Lead us not into temptation, but deliver us from evil. Amen.
HAIL MARY.
Hail Mary, full of grace; the Lord is with thee. Blessed art thou among women, and blessed is Jesus, the fruit of thy womb.
Holy Mary, Mother of God, pray for us sinners, now and at the hour of our death. Amen.
ACT OF FAITH.
My God, I believe all the truths believed and taught by the Roman Catholic Church, because you have revealed them to us. You are not deceived, and you do not deceive. Amen.
ACT OF HOPE.
My God, I hope in you, that through Jesus Christ I will be given your graces here on earth and glory in Heaven, because you have promised these things to us and you are faithful. Amen.
ACT OF LOVE.
My God, I love you above all things, because you are good and lovable. I love my neighbor as myself for your sake. Amen.
CONFESSION OF SINS.
Let us think in our hearts of all the sins of today by which we have offended God, in thought, word, and deed (………………………)
I confess to Almighty God, and to you, my brothers and sisters, that I have greatly sinned, in my thoughts, in my words, in my actions, and in failing to fulfill my duty. I have sinned, I have sinned, I have greatly sinned. Therefore I ask blessed Mary ever Virgin, the angels and all the saints, and you, my brothers and sisters, to pray for me to the Lord our God.
+May Almighty God have mercy on us, forgive us our sins, and bring us to everlasting life. Amen.
ACT OF CONTRITION.
My God, I am very sorry for the sins I have committed against you, because you are good and lovable. Sin displeases you, so I do not want to sin again. I will do penance; I ask your grace so that I may return. Amen.
O merciful God, pour out your blessings upon our Holy Father Francis, the bishops, priests, deacons, farmers, all workers, students, and the whole community whom you make your people. Save those who do not yet know you, comfort the sick, and guide those who are dying so they may see the light of eternity. Amen.
ANGELUS.
The Angel of the Lord declared unto Mary, and she conceived by the power of the Holy Spirit.
~Hail Mary, full of grace; the Lord is with thee. Blessed art thou among women, and blessed is Jesus, the fruit of thy womb. Holy Mary, Mother of God, pray for us sinners, now and at the hour of our death. Amen.
Behold the handmaid of the Lord; be it done unto me according to your word.
~Hail Mary, full of grace; the Lord is with thee. Blessed art thou among women, and blessed is Jesus, the fruit of thy womb. Holy Mary, Mother of God, pray for us sinners, now and at the hour of our death. Amen.
And the Word of God was made flesh and dwelt among us.
~Hail Mary, full of grace; the Lord is with thee. Blessed art thou among women, and blessed is Jesus, the fruit of thy womb. Holy Mary, Mother of God, pray for us sinners, now and at the hour of our death. Amen.
Pray for us, O Holy Mother of God, that we may be made worthy of the promises of Christ.
Let us pray:
Pour forth, we beseech you, O Lord, your grace into our hearts, that we to whom the incarnation of Christ your Son was made known by the message of an angel may, by his Passion and Cross, be brought to the glory of the Resurrection.
We ask this through Christ our Lord.
Mary, Queen of Peace ~ Pray for us!
PRAYER TO THE GUARDIAN ANGEL.
My guardian angel, protect me from all dangers of soul and body. Amen.
Glory be to the Father, and to the Son, and to the Holy Spirit. As it was in the beginning, is now, and ever shall be, world without end. Amen.